Usalama kuimarishwa kabla ya mazishi ya mwendazake Ong'ondo Were hapo kesho

Friday, 9 May, 2025

Usalama kuimarishwa kabla ya mazishi ya mwendazake Ong'ondo Were hapo kesho

Kaunti ya Homabay
Alhamisi Mei 8, 2025

Wito wa amani na utulivu umetolewa kabla ya mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa Kasipul, Charles Ong’ondo Were, huku maandalizi ya mwisho yakiendelea katika Shule ya Sekondari ya Agoro Sare ambako watu walikusanyika kwa maombi, mahubiri, na kutazama mwili wa marehemu kwa mara ya mwisho.

Viongozi wa kisiasa wakiongozwa na Kamishna wa Tume ya Huduma za Bunge (PSC), Mishi Mboko, walitoa wito wa kuimarishwa kwa usalama kutokana na hofu ya kuwepo kwa watu wanaopanga kuvuruga shughuli za mazishi kwa fujo.

Mbunge huyo ambaye aliheshimiwa kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya eneo la Kasipul, anatarajiwa kuzikwa kesho kwa heshima kubwa. Wakazi wa Kasipul wametakiwa kudumisha amani na kuenzi maisha ya Were kwa kutokubali kushiriki au kuunga mkono vurugu zozote.

“Hili ni tukio la heshima. Tujiepushe na chokochoko za kisiasa na tutumie fursa hii kumuenzi kiongozi wetu kwa amani,” alisema Mboko.

Mazishi hayo yanatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi wa kitaifa na wa kaunti pamoja na wananchi kwa ujumla


Usalama kuimarishwa kabla ya mazishi ya mwendazake Ong'ondo Were hapo kesho

MORE UPDATES

  • Parliament Begins Funeral Arrangements for Late Ol Kalou MP Hon. David Kiaraho
    Parliament Begins Funeral Arrangements for Late Ol Kalou MP Hon. David
  • Committee to Probe Seven Entities As It Probes Alleged Loss Of Sh9billina From E-Citizen
    Committee to Probe Seven Entities As It Probes Alleged Loss Of Sh9billina
  • House committee steps up peace drive in Isiolo County.
    House committee steps up peace drive in Isiolo County.
  • Nationwide Public Participation Exercise On The Public Participation Bill
    Nationwide Public Participation Exercise On The Public Participation Bill
  • No Charlatans Will Be Allowed To Operate In Kenya, Public Work Ps Assures Housing Committee
    No Charlatans Will Be Allowed To Operate In Kenya, Public Work Ps Assures
  • Address Bomayangu Platform Bottlenecks, Housing Committee Tells State Department
    Address Bomayangu Platform Bottlenecks, Housing Committee Tells State